Friday, December 19, 2014
On 8:45 AM by Unknown No comments

Siku mbili baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji
Frederick Werema, kujiuzulu, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,
Prof. Anna Tibaijuka, ameibuka na kusema yeye pamoja na Waziri wa Nishati na
Madini, Prof. Sospeter Muhongo, hawawezi kuchukua uamuzi huo kwa sababu Rais
Jakaya Kikwete anawategemea kwa uchapaji kazi wao.
Prof. Tibaijuka na Prof. Muhongo, ni miongoni mwa watuhumiwa wa kashfa ya uchotwaji wa zaidi ya Sh. bilioni 300 katika akaunti ya Tegeta Escrow, iliyokuwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
Wengine ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi; Jaji Werema; Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge; Mbunge wa Lupa (CCM), Victor Mwambalaswa na Mbunge wa Sengerema (CCM), William Ngeleja.
Prof. Tibaijuka alitoa msimamo huo alipozungumza na waandishi wa habari katika mkutano ulioitishwa ghafla jijini Dar es Salaam jana.
Alisema yeye na Prof. Muhongo wanafanya kazi kubwa, ambayo inamfanya Rais Kikwete awategemee na kwamba, wanafahamiana walipokuwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
“Kazi za Muhongo alizopewa na Rais Kikwete zinaonekana kwa macho, kama nguzo za umeme, wananchi wanaona. Lakini kazi zangu hazionekani. Ni kama figo zilizoko ndani ya mwili wa binadamu. Kazi ya Wizara ya Ardhi ni kubwa kuliko watu wanavyofikiri,” alisema Prof. Tibaijuka.
Akijibu swali kama yeye ni kibaraka wa Prof. Muhongo kutokana na kupata mgawo katika fedha hizo, alisema yeye (Prof. Tibaijuka) hawezi kuwa kibaraka na hawezi kufanya kazi ya udalali.
Alisema yeye na Prof. Muhongo wanafahamiana na kwamba, hata Rais Kikwete anafahamu urafiki wao na hawawezi kuacha kushirikiana kwa sababu wote wamepewa kazi na Rais, ambaye atashangaa kusikia hawaongei.
Prof. Tibaijuka, ambaye alipata mgawo wa Sh. bilioni 1.6 katika fedha hizo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya VIP Engineering and Marketing LTD, James Rugemalira, alisema kamwe hawezi kujiuzulu na pia anajivunia na kuona fahari kupata fedha hizo. Kampuni hiyo ya Rugemalira ilikuwa mwana hisa katika IPTL.
Alisema ni bora alivyopata fedha hizo na kuzipeleka katika shule yake kwa ajili ya kusaidia shughuli za elimu kwa watoto wa kike wasio na uwezo.
Kutokana na hali hiyo, alisema anahitaji kusifiwa kwa ujasiri wake wa kukiri kupokea fedha hizo na kuzitolea maelezo, ingawa alikosa nafasi hiyo katika Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC).
Akijibu swali sababu za kutokutoa maelezo hayo mbele ya PAC, Prof. Tibaijuka alisema anayepaswa kuulizwa swali hilo ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya Bunge, Zitto Kabwe.Alisema PAC haikumwita ili atoe maelezo hayo, badala yake Bunge liliishia kutoa maazimio, ambayo mawili kati yake, moja likitaka wachunguzwe na lingine wawajibishwe.Prof. Tibaijuka alisema wakati azimio la kutaka wachunguzwe halijatekelezwa, azimio la kutaka wawajibishwe tayari linatoa hukumu dhidi yao.
Akijibu swali sababu za kugoma kujiuzulu, alisema fedha hizo hazijathibitishwa kuwa ni haramu.Alisema atajiuzulu tu iwapo itathibitika fedha hizo za Rugemalira, siyo halali.
Prof. Tibaijuka alisema fedha hizo hazijathibitishwa na serikali kuwa siyo halali, kiasi cha yeye kutakiwa kujiuzulu nafasi yake serikalini.Alisema fedha hizo hazina uhusiano kati yake na nafasi ya uwaziri aliyonayo, kwani zilikwenda moja kwa moja kusaidia kulipa deni la Sh. bilioni mbili, ambazo moja ya shule zake ilikopo kutoka Benki M.
Prof. Tibaijuka alisema iwapo itabainika fedha hizo si halali atakuwa tayari kuzirudisha.“Iwapo fedha hizo zitathibitika siyo halali, Joha Trust itazirudisha, kama taasisi inavyoitwa nia njema, sisi hatuhifadhi fedha zisizo halali,” alisema Prof. Tibaijuka.
Alisema fedha hizo alizipokea Februari 12, mwaka huu, zilitokana na maombi ya awali kutafuta michango kutoka kwa wafanyabiashara wa ndani na wafadhili wa nje.Alisema hoja kwamba, alipokea mchango mkubwa, haina uzito kutokana aina ya mtu, ambaye alimpa mchango huo na kusema ni mtu mwenye fedha na pia ni mfanyabiashara.
“Labda mnafikiri unapoomba fedha kwa mtu kama Bill Gates unategemea atakuchangia kama kiasi gani? Siyo senti. Hata mimi nilipoambiwa na Rugemalira nikaangalie akaunti yangu ina shilingi ngapi na kukuta fedha nyingi, nilijua leo nimeamkia mkono wa kulia. Nilifurahi,” alisema Prof. Tibaijuka.
Alisema fedha hizo alichangiwa kwa ajili ya kulipa sehemu ya deni la Sh. bilioni mbili anazodaiwa na Benki M.Prof. Tibaijuka alisema fedha hizo walikopa kwa ajili ya ujenzi wa bweni la shule lenye uwezo wa vitanda 163.
Alisema fedha hizo zimechangia maendeleo ya elimu kwa kuwatengenezea watoto mazingira bora.“Hii kitu inabidi tuwe makini kama Taifa, kwani mimi nilikuwa mtumishi Umoja wa Mataifa. Lakini sikuweza kubeba fedha. Na kuna mapesa kule. Iwe katika nchi hii, ambayo nafahamu hata wapigakura wangu wa kule Muleba Kusini na wakulima wanaishi maisha ya chini?” alihoji Prof. Tibaijuka.
Alisema uamuzi wa kuzitoa fedha hizo haraka katika Benki ya Mkombozi, ulifikiwa na Bodi ya Wadhamini ya Joha Trust, ambayo ilitoa maamuzi kwamba, zitumike kulipa deni la Benki M.Hata hivyo, katika mkutano huo Prof. Tibaijuka hakutoa nyaraka zozote zikiwamo risiti zinazoonyesha deni hilo lilivyolipwa kupitia benki hiyo.
Alisema analazimika kutoa maelezo hayo katika vyombo vya habari kutokana na kutopewa nafasi ya kufanya hivyo mbele ya PAC.
“Kitendo cha mimi kuitwa Escrow, kwa kweli si kizuri na kinashusha maadili hata ya wewe unayekifanya. Waandishi msiandike, ambacho kinasemwa. Fuatilieni kwa umakini. Kwanza hii inaweza kuliweka Taifa katika image (taswira) mbaya. Nilitumikia Umoja wa Mataifa (UN), hata Katibu Mkuu wa UN akiona nimechukua fedha hizi hii, haipendezi,” alisema Prof. Tibaijuka.
Alisema serikali bado haijathibitisha kuwa fedha za Rugemalira ni haramu kiasi cha yeye kulaumiwa.Kutokana na hali hiyo, alionya kuwa kujiuzulu kusiwe kama mtindo, kwani fedha hizo hazikugusa utendaji kazi wake kama mtumishi wa serikali.Alisema mitandao inaendelea kuandika na asilimia kubwa wakimtukana.
Matamshi hayo yametolewa na Prof. Tibaijuka katika kipindi, ambacho Rais Kikwete akitarajiwa kutoa maamuzi kuhusiana na kashfa hiyo wakati wowote.Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, jijini Dar es Salaam, Jumapili ya wiki iliyopita, Rais Kikwete anatarajiwa kutoa maamuzi hayo ndani ya wiki hii.
Prof. Tibaijuka na Prof. Muhongo, ni miongoni mwa watuhumiwa wa kashfa ya uchotwaji wa zaidi ya Sh. bilioni 300 katika akaunti ya Tegeta Escrow, iliyokuwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
Wengine ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi; Jaji Werema; Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge; Mbunge wa Lupa (CCM), Victor Mwambalaswa na Mbunge wa Sengerema (CCM), William Ngeleja.
Prof. Tibaijuka alitoa msimamo huo alipozungumza na waandishi wa habari katika mkutano ulioitishwa ghafla jijini Dar es Salaam jana.
Alisema yeye na Prof. Muhongo wanafanya kazi kubwa, ambayo inamfanya Rais Kikwete awategemee na kwamba, wanafahamiana walipokuwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
“Kazi za Muhongo alizopewa na Rais Kikwete zinaonekana kwa macho, kama nguzo za umeme, wananchi wanaona. Lakini kazi zangu hazionekani. Ni kama figo zilizoko ndani ya mwili wa binadamu. Kazi ya Wizara ya Ardhi ni kubwa kuliko watu wanavyofikiri,” alisema Prof. Tibaijuka.
Akijibu swali kama yeye ni kibaraka wa Prof. Muhongo kutokana na kupata mgawo katika fedha hizo, alisema yeye (Prof. Tibaijuka) hawezi kuwa kibaraka na hawezi kufanya kazi ya udalali.
Alisema yeye na Prof. Muhongo wanafahamiana na kwamba, hata Rais Kikwete anafahamu urafiki wao na hawawezi kuacha kushirikiana kwa sababu wote wamepewa kazi na Rais, ambaye atashangaa kusikia hawaongei.
Prof. Tibaijuka, ambaye alipata mgawo wa Sh. bilioni 1.6 katika fedha hizo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya VIP Engineering and Marketing LTD, James Rugemalira, alisema kamwe hawezi kujiuzulu na pia anajivunia na kuona fahari kupata fedha hizo. Kampuni hiyo ya Rugemalira ilikuwa mwana hisa katika IPTL.
Alisema ni bora alivyopata fedha hizo na kuzipeleka katika shule yake kwa ajili ya kusaidia shughuli za elimu kwa watoto wa kike wasio na uwezo.
Kutokana na hali hiyo, alisema anahitaji kusifiwa kwa ujasiri wake wa kukiri kupokea fedha hizo na kuzitolea maelezo, ingawa alikosa nafasi hiyo katika Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC).
Akijibu swali sababu za kutokutoa maelezo hayo mbele ya PAC, Prof. Tibaijuka alisema anayepaswa kuulizwa swali hilo ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya Bunge, Zitto Kabwe.Alisema PAC haikumwita ili atoe maelezo hayo, badala yake Bunge liliishia kutoa maazimio, ambayo mawili kati yake, moja likitaka wachunguzwe na lingine wawajibishwe.Prof. Tibaijuka alisema wakati azimio la kutaka wachunguzwe halijatekelezwa, azimio la kutaka wawajibishwe tayari linatoa hukumu dhidi yao.
Akijibu swali sababu za kugoma kujiuzulu, alisema fedha hizo hazijathibitishwa kuwa ni haramu.Alisema atajiuzulu tu iwapo itathibitika fedha hizo za Rugemalira, siyo halali.
Prof. Tibaijuka alisema fedha hizo hazijathibitishwa na serikali kuwa siyo halali, kiasi cha yeye kutakiwa kujiuzulu nafasi yake serikalini.Alisema fedha hizo hazina uhusiano kati yake na nafasi ya uwaziri aliyonayo, kwani zilikwenda moja kwa moja kusaidia kulipa deni la Sh. bilioni mbili, ambazo moja ya shule zake ilikopo kutoka Benki M.
Prof. Tibaijuka alisema iwapo itabainika fedha hizo si halali atakuwa tayari kuzirudisha.“Iwapo fedha hizo zitathibitika siyo halali, Joha Trust itazirudisha, kama taasisi inavyoitwa nia njema, sisi hatuhifadhi fedha zisizo halali,” alisema Prof. Tibaijuka.
Alisema fedha hizo alizipokea Februari 12, mwaka huu, zilitokana na maombi ya awali kutafuta michango kutoka kwa wafanyabiashara wa ndani na wafadhili wa nje.Alisema hoja kwamba, alipokea mchango mkubwa, haina uzito kutokana aina ya mtu, ambaye alimpa mchango huo na kusema ni mtu mwenye fedha na pia ni mfanyabiashara.
“Labda mnafikiri unapoomba fedha kwa mtu kama Bill Gates unategemea atakuchangia kama kiasi gani? Siyo senti. Hata mimi nilipoambiwa na Rugemalira nikaangalie akaunti yangu ina shilingi ngapi na kukuta fedha nyingi, nilijua leo nimeamkia mkono wa kulia. Nilifurahi,” alisema Prof. Tibaijuka.
Alisema fedha hizo alichangiwa kwa ajili ya kulipa sehemu ya deni la Sh. bilioni mbili anazodaiwa na Benki M.Prof. Tibaijuka alisema fedha hizo walikopa kwa ajili ya ujenzi wa bweni la shule lenye uwezo wa vitanda 163.
Alisema fedha hizo zimechangia maendeleo ya elimu kwa kuwatengenezea watoto mazingira bora.“Hii kitu inabidi tuwe makini kama Taifa, kwani mimi nilikuwa mtumishi Umoja wa Mataifa. Lakini sikuweza kubeba fedha. Na kuna mapesa kule. Iwe katika nchi hii, ambayo nafahamu hata wapigakura wangu wa kule Muleba Kusini na wakulima wanaishi maisha ya chini?” alihoji Prof. Tibaijuka.
Alisema uamuzi wa kuzitoa fedha hizo haraka katika Benki ya Mkombozi, ulifikiwa na Bodi ya Wadhamini ya Joha Trust, ambayo ilitoa maamuzi kwamba, zitumike kulipa deni la Benki M.Hata hivyo, katika mkutano huo Prof. Tibaijuka hakutoa nyaraka zozote zikiwamo risiti zinazoonyesha deni hilo lilivyolipwa kupitia benki hiyo.
Alisema analazimika kutoa maelezo hayo katika vyombo vya habari kutokana na kutopewa nafasi ya kufanya hivyo mbele ya PAC.
“Kitendo cha mimi kuitwa Escrow, kwa kweli si kizuri na kinashusha maadili hata ya wewe unayekifanya. Waandishi msiandike, ambacho kinasemwa. Fuatilieni kwa umakini. Kwanza hii inaweza kuliweka Taifa katika image (taswira) mbaya. Nilitumikia Umoja wa Mataifa (UN), hata Katibu Mkuu wa UN akiona nimechukua fedha hizi hii, haipendezi,” alisema Prof. Tibaijuka.
Alisema serikali bado haijathibitisha kuwa fedha za Rugemalira ni haramu kiasi cha yeye kulaumiwa.Kutokana na hali hiyo, alionya kuwa kujiuzulu kusiwe kama mtindo, kwani fedha hizo hazikugusa utendaji kazi wake kama mtumishi wa serikali.Alisema mitandao inaendelea kuandika na asilimia kubwa wakimtukana.
Matamshi hayo yametolewa na Prof. Tibaijuka katika kipindi, ambacho Rais Kikwete akitarajiwa kutoa maamuzi kuhusiana na kashfa hiyo wakati wowote.Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, jijini Dar es Salaam, Jumapili ya wiki iliyopita, Rais Kikwete anatarajiwa kutoa maamuzi hayo ndani ya wiki hii.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Search
Translate
Popular Posts
-
Leo wanawake wenzangu kwenye safu yetu hii pendwa nimewaletea mada moja nzito ambayo ukiiendekeza unavunja nyumba yako hivihivi unajiona.H...
-
Utandawazi utawaabisha wengi kwani hizi simu zetu ukizubaa kidogo mtu anakupiga picha hata kama hujadhamiria kufanya hivi.
-
Stori: Chande Abdallah na Deogratius Mongela AIBU ilioje! Denti wa chuo kimoja jijini Dar, anayefahamika kwa jina moja la Martha, amepiga...
-
Hebu niambie...umeshawahi kujichua? Mara ngapi? Bado unaendelea na mchezo huo? Vipi, umewahi kusikia watu wakizungumza kuhusu suala hilo? ...
-
Wanachuo wazidi kuwa mfano mbaya licha kuonekana wasomi na ndio tegemeo kwa taifa la kesho lakini cha ajabu wanazidi kufanya madudu badal...
-
MDADA MWENYEWE NI HUYU. DENT mmoja katika Chuo Kikuu kimojawapo hapa nchini amepiga picha zisizo na maadili akiwa na njemba wake katika ...
-
Kweli dunia inamambo watu kadhaa wamekamatwa na kamera zetu wkingonoka bila uoga wowote tena hadharani hebu ona picha hapa
-
Hivi Majuzi mke wa Mchungaji mmoja amekamatwa laivu akingonoka vichakani umbali kidogo kutoka katika nyumbani kwake Mke wa Mchungaji a...
-
Polisi mkoani Tanga wamesema wataendesha msako wa kuwakamata watu wanaofanya biashara ya ngono katika nyumba za starehe na mitaa maarufu ...
Blog Archive
-
▼
2014
(168)
-
▼
December
(168)
- BAADA YA KIMYA CHA MUDA MREFU MREMBO RAYUU AIBUKA ...
- Polisi Yatangaza Msako kwa Wanawake Wanaofanya Bia...
- Nimeamua Kutoka Kimapenzi na Binti wa Kazi ( Hausi...
- Samantha Apokelewa Kwa Mikono Miwili na Familia ya...
- PHOTO’S: HIVI NDIVYO ALIVYOPOKELEWA DIAMOND NA KUN...
- SIMBA YAFUKUZA MAKOCHA
- DIAMOND PLATNUMZ ATUA RWANDA KWA SHANGWE
- WAIMBA INJILI WANA NINI?
- MWANAMKE ADAIWA KUTEKA WATOTO
- BASTOLA TISHIO DAR!
- VANESSA AWATOA KIMASOMASO WASANII WA KIKE
- Bilionea wa Nigeria ampiku Oprah na kuwa mwanamke ...
- Mvua Yaua Jijini Dar.....Mtoto Asombwa na Maji aki...
- Binti Ajizalisha na kutumbukiza mtoto kwenye ndoo
- Mgombea urais atabiriwa kifo.....Yadaiwa Atafariki...
- Washitakiwa mauaji ya Dk Mvungi wazua kizaazaa mah...
- Hili ni Fundisho Kwa Wanaume Wanaopenda Kutongoza ...
- MAKAVU LIVE!!!:: UTAMU WA MUA UKIKUTANA NA KIFUNDO...
- Wajua Jinsi ya Kumdhibiti Mpenzi Anayepiga Mizinga?
- PICHA ZA UTAMU ZA DENTI WA CHUO KIKUU CHA UDOM ZAN...
- Bi dada... Utafanya nini? Mmeo Anatembea na binti ...
- Waziri Nyalandu atangaza nia ya kuwa Rais wa Tanzania
- Kashfa ya Escrow ndo sababu kuu ya Anguko la CCM-W...
- Tibaijuka: Nitagombea Ubunge Mwakani licha ya Saka...
- Mwenyekiti wa CHADEMA Atimuliwa nchini kwa madai k...
- UCHAWI:BIBI KIZEE AKUTWA KAANGUKA NJE YA KANISA AS...
- TAZAMA JINSI SIKUKUU YA KRISMAS INAVYOENDELEA KATI...
- BAADA YA KIMYA KIREFU MSANII 'Q CHIEF' SASA KUACHA...
- LAANA YA SIKU : :VIJANA WAFANYA USHENZI KUPITILIZA
- LAANA..!!! BOFYA UONEE VIZURII DADA HUYU ALIVYOAMU...
- PICHA ZA UCHI ZA MSANII MAARUFU WA KIKE AKILIWA TI...
- ZAIDI YA LAANA: HUU NDIOUCHAFU ULIOFANYIKA JANA KW...
- RAIS OBAMA AITWA TUMBILI NA KOREA KASKAZINI!
- DAVINA:STEVE NYERERE NI MTU POA ILA ANA VIMATATIZO...
- DIAMOND PLATNUMZ HANA UWEZO WA KUMPA MWANAMKE UJAU...
- KAKA NA DADA WANASWA LAIVU WAKIFANYA MAPENZI,WAFAN...
- MAJANGA !!! MKE WA MTU AWEKA PICHA CHAFU KATIKA UK...
- WASTARA KUMUANIKA MRITHI WA SAJUKI
- Hizi Ndizo Sifa Za Mtu Anayefaa Kuwa Rais Ajaye ,W...
- Dunia Imeisha Tizama Picha Za Hawa Wadada Walizopo...
- DAVIDO ALA DENDA NA SHABIKI AKIWA STEJINI!!!
- DUNIA IMEKWISHA CHEKI PICHA YA MCHUMBA WA MTU AKIN...
- AFARIKI DUNIA BAAADA YA KULIPULIWA NA BOMU ALILOTA...
- HILI NI FUNDISHO KWA WAKE ZA MARAISI AFRIKA!!!HUYU...
- LIPUMBA NA ZITTO KABWE WAPANGA KUWASHA MOTO WA ESC...
- HIVI NDIVYO TIBAIJUKA ALIVYOTEMA CHECHE HUKO JIMBO...
- HIVI UNAFAHAMU KUWA LIPUMBA ALISHAWAHI KUWA MSAIDI...
- BUBU Afanyiwa Unyama wa Kutisha......Wanaume Watan...
- Hausiboi Aliyelawiti Mtoto wa Miaka 6 Ahukumiwa Ki...
- BAKWATA Yasisitiza kuwa Maamuzi ya Rais Kikwete ku...
- Matokeo Mabaya ya CCM Singida: Nyalandu Abebeshwa ...
- HII NI NOMA..!! JIONEE PICHA 15 ZA HUYU MZUNGU ALI...
- JINSI YA KUJIZUIA USIKOJOE MAPEMA NA HIVYO KUSHIND...
- Krismasi ni Escrow kila kona
- Vijana Watatu Wakamatwa Wakijaribu Kuiba Sanamu ya...
- Rais Kikwete atakiwa kuwachukulia hatua Mawaziri W...
- CCM yaongoza matokeo ya jumla serikali za mitaa
- Ukawa Mkilifanya Hili, 2015 Mnashinda kwa Zaidi ya...
- Ray C: Nina uhakika Alikiba Akipata Support ya Dia...
- Panapo Fuka Moshi Kuna Moto..Habari za Millard Ayo...
- Bifu la Davido na Wizkid Limeisha, La Ally Kiba na...
- Sserunkuma atupia mbili, aonyesha cheche Zenji
- SAFARI YA MABALOZI KUPANDA MLIMA KILIMANJARO KATIK...
- VODACOM TANZANIA ILIVYOWARUSHA WATEJA WAKE KILA KO...
- Waziri Muhongo aanza Ziara ya Siku 6 Mkoani Mara k...
- MADAWA YA KULEVYA HATARI ZAIDI KWA WASANII
- KUNDI LILILOPATA PIGO ZAIDI 2012-14
- SHOO YA DIAMOND DAR LIVE YAACHA HISTORIA
- R.I.P WASANII WETU! KINACHOWAUA KWA KASI CHAJULIKANA
- FAIZA: MIMI SIYO MBULULA KWA KUVAA PEMPASI
- BALAA LA KRISMASIMREMBO APOTEZA FAHAMU
- DUH!! JE WAJUA KILICHOMPATA MENEJA WA CLOUDS JUU Y...
- AIBU YA MWAKA!!!!!! TAZAMA ALICHOFANYIWA DADA HUYU...
- PICHA ZA WATU WAZIMA WAKINGONOKA HADHARANI HII NI ...
- TAMASHA LA TUONANE JANUARY (TUO8 JANUARY) LAFANA M...
- JINSI YA KUMTOA MWANAMKE BIKRA BILA MAUMIVU ........
- Diamond Aeleza Demu Aliemtungia Wimbo Wake Mpya Wa...
- Ona Mama Diamond Jinsi Anavoonekana Kuwa Chanzo Ch...
- FUMANIZI!!! PATA KUONA ALICHOFANYIWA DADA HUYU BAA...
- MJUE MKE MTARAJIWA WA MASANJA MKANDAMIZAJI!, IONE ...
- WANACHUO WANAOPIGA PICHA ZA UTUPU WAZIDI KUONGEZEK...
- Baadhi ya Picha za Wema na Van Vicker Wakiwa Katik...
- Nimeamini, Mabinti wa Kichaga Hawajui Mapenzi Hata...
- Wavulana Ma-handsome Hawana Lolote Kitandani..Kazi...
- Yamenikuta: Mchumba wangu amezaa angali bikra
- Rais Kikwete Akutana na Msanii Diamond Platnumz Ik...
- JOKATE: SIJAWAHI KUROGA ILI NIFANIKIWE
- WEWE TIBAIJUKA! JEMBE LISILOLIMA LINA FAIDA GANI?
- DIAMOND AANIKA SABABU 5 ZA KUMPENDA ZARI!
- Wema Sepetu Apandishwa Kizimbani
- Mume Ajinyonga Ukweni baada ya Mkewe Kumkataa
- Baada ya Kupotea Kwa Muda Mrefu Agness Masogange A...
- Headmistress Caught Being Banged By Her Watchman I...
- Wema Ampongeza Jokate Lakini Asisitiza Kuendelea K...
- Magazeti ya Leo Jumatatu ya tarehe 22 Disemba 2014
- Mke wa Mtu Anaswa Akijiuza Kusaka Pesa za Christmass
- Diamond: Aliyenifundisha Kuongea Kiingereza ni Pen...
- CHADEMA Watoa Tahadhari kwa Rais kuhusu Kuwatetea ...
- MTOTO WA JACKIE CHAN ASHITAKIWA KWA DAWA ZA KULEVYA
- MWENYEKITI WA PROIN, JOHNSON LUKAZA NA MDOGO WAKE ...
-
▼
December
(168)
0 comments:
Post a Comment